Tuesday, March 30, 2010

Ni wakati gani mazoezi hayaruhusiwi kwenye ujauzito?


Kwa mujibu wa maelekezo yaliyotolewa na Chuo Kikuu Cha Marekani cha Masuala ya Uzazi na Magonjwa ya Wanawake, mama mjamzito haruhusiwi kufanya mazoezi iwapo atakuwa na matataizo yafuatayo:
• Ugonjwa wa moyo.
• Ugonjwa wa mapafu.
• Kizazi kisichojitocheleza au kitaalamu cervical insufficiency/cerclage.
• Mimba ya mapacha, mapacha wawili, watatu na kuendelea na iwapo ana hatari ya kujifungua mapema kabla ya muda kutimia.
• Kutokwa na damu kunakoendelea katika miezi mitatu ya pili na ya tatu ya mimba.





• Mfuko wa uzazi ulioko upande wa chini wa kizazi au placenta previa. Hasa baada ya wiki 26 ya mimba.
• Uwezekano wa kujifungua mapema kabla muda haujatimia.
• Iwapo chupa imevunjika.
• Kifafa cha mimba (preeclamsia)
• Shinikizo sugu la damu.
• Ukosefu mkubwa wa damu.
• Kutokwa na majimaji ukeni.
• Ongezeko la mapigo ya moyo, hata wakati wa mapumziko.

No comments: