Monday, February 15, 2010

Wanawake wenye umri zaidi ya miaka 35 wasisahau kuzuia mimba, umri sio tija!


Wataalamu wamewapa tahadhari wanawake wenye umri mkubwa kwamba wasijisahau kutumia dawa za kuzuia uzazi, wakiamini kimakosa kwamba hawawezi kupata mimba kwa kuwa wamepitisha umri wa kubeba mimba. Wataalamu wanasema kuwa, ingawa kiwango cha ubebaji mimba hupungua kadri umri wa mwanamke unavyopita miaka 30 lakini haimaanishi kwamba wanawake hao hawawezi kubeba mimba wakiwa katika miaka ya 40 au 50. Imeonekana kuwa watu wengi wakipitisha miaka 35 hujisahau na kudhani kwamba hawawezi kupata mimba tena na hivyo huacha kutumia njia za kuzuia mimba suala ambalo limesababisha kiwango cha utoaji mimba katika nchi za Maghribi kama vile Uingereza kwa wanawake wenye umri wa miaka 40 hadi 44 kiwe sawa na cha wasiachana walio chini ya miaka 16. Kuna sababu nyingi zinazowapelekea baadhi ya wanawake waamue kutoa mimba, mojawapo ni kuhofia hatari ya kuzaa watoto wenye matatizo (abnormalities) tatizo ambalo hutokea sana kwa wanawake wanaobeba mimba katika umri mkubwa. Lakini wataalamu wanasema kwamba sababu nyingineyo ni wanawake waliobeba mimba bila kujua kwa kuwa walidhani hawatapata mimba kwa kuwa wana umri mkubwa. Kwa ajili hiyo madakatari wanawashauri wanawake wote waliofikisha miaka 35 na kuendelea wachukue tahadhari kuhusiana na mimba zisizopangwa na waendelee kutumia njia mbalimbali za kuzuia uzazi hadi pale wanapofikia kukoma hedhi au menopause, iwapo hawataki kupata watoto.
Kwa kawaida kitaalamu umri mzuri wa kubeba mimba ni kati ya miaka 20 hadi 35. Kubeba mimba kabla ya miaka 20 huweza kuhatarisha maisha ya mama na mtoto kutokana na sababu mbalimbali za kiafya, kisaikolojia na kiuchumi na kubebea mimba baada ya miaka 35 nako kuna uwezekano mkubwa wa kuhatarisha maisha ya mama na mtoto. Mimba zinazobebwa baada ya miaka 35 hambatana na matatizo mbalimbali kama vile shinikizo la damu, kifafa cha ujauzito, kisukari cha ujauzito na kadhalika huku mtoto anayezaliwa akiwa na uwezekano mkubwa wa kuwa na matatizo ya kuzaliwa (abnormalities). Wataalamu wanashauri kuwa iwapo utapata mimba baada ya miaka 35 ni vyema ufanyiwe baadhi ya vipimo wakati mimba bado ni ndogo ili kujua iwapo mtoto aliye tumboni ana matatizo au la.

3 comments:

Anonymous said...

wanawake WALIOA....KWELI???????

Shally's Med Corner said...

thanks... namaanisha walio na... lol ni matatizo ya uandishi. thanks !

Anonymous said...

Sikuwahi kuamini kitu kama hiki kingeweza kunitokea hadi ndoa yangu ilipokaribia kuisha kabisa.

Mume wangu alibadilika ghafla. Mwanaume ambaye hapo awali alinipenda na kunijali akawa baridi, asiyejali, na mwenye hasira bila sababu. Aliacha kuonyesha nia katika ndoa yetu, akaniepuka kabisa, na hatimaye akaniomba talaka. Nilivunjika moyo kwa sababu nilimpenda mume wangu kwa moyo wangu wote.
Mambo yalizidi kuwa mabaya aliponizuia kila mahali — WhatsApp, Facebook, Instagram — kana kwamba sijawahi kuwepo. Nililia kila usiku nikijiuliza nilifanya nini kibaya.
Siku moja, rafiki wa karibu alinitembelea na kunitambulisha kwa mtu wa kiroho anayeitwa Dkt. Dawn. Kwa kweli, mwanzoni nilikuwa na shaka, lakini niliamua kumweleza kila kitu kwa sababu sikuwa na chochote cha kupoteza.

Dkt. Dawn alinisomea mambo ya kiroho, na nilishtuka. Alifichua siri kuhusu ndoa yangu na maisha yangu binafsi ambayo hakuna mtu aliyejua. Kila kitu alichosema kilikuwa sahihi 100%. Kisha akafichua kwamba mwanamke mwingine alikuwa amemloga mume wangu. Mwanamke huyu alikuwa akimtembelea mara nyingi, na kwa upumbavu niliamini ilikuwa kuhusu kazi tu.
Dkt. Dawn alinisaidia kuvunja uchawi na akafanya ibada yenye nguvu ya kurejesha upendo kwa ndoa yangu.
Kwa mshangao wangu mkubwa, muda mfupi tu baadaye, mume wangu alinifungulia kizuizi mwenyewe na kuanza kunipigia simu na kunitumia ujumbe mwingi, akiniomba nimsamehe na nirudi nyumbani. Mwanzoni nilimpuuza kwa sababu ya maumivu aliyonisababishia, lakini hatimaye alirudi nyumbani akiwa na zawadi na machozi machoni mwake akiomba nafasi nyingine.
Leo, ndoa yetu ni imara zaidi, yenye furaha zaidi, na yenye amani zaidi kuliko hapo awali. Mapenzi kati yetu yanahisi upya kabisa.
Kana kwamba hiyo haitoshi, Dkt. Dawn baadaye alinisaidia na ibada ya ujauzito kwa sababu tulikuwa tumejitahidi kwa miaka mingi kupata watoto. Ndani ya wiki 8, nilipata mimba kiasili, na leo tumebarikiwa na wavulana wawili wazuri wenye afya njema.
Nitaendelea kushukuru milele.
Ukihitaji: Uchawi wa mapenzi wa kuungana tena na mpenzi wako wa zamani
. Usaidizi wa kurejesha ndoa
. Tamaduni za ujauzito za kupata mimba
. Usaidizi wa kiroho kwa kesi za mahakamani au kupona urithi
. Mwongozo na ulinzi wa kiroho
Ninapendekeza sana Dkt. Dawn. Ushuhuda wangu ni wa kweli, na furaha yangu leo ni uthibitisho. WhatsApp yake: +2349046229159. dawnacuna314@gmail.com