Friday, September 11, 2009

Kuishi maisha mazuri kunapunguza hatari ya kupata saratani ya matiti


Utafiti mpya umeonyesha kuwa, kuishi maisha mazuri na kunyonyesha mtoto kunaweza kuazuia kesi 70, 000 za kensa ya matiti kila mwaka.
Ripoti iliyotolewa na Taasisi ya Marekani ya Wataalamu wa Uchunguzi wa Saratani Duniani imeonyesha kuwa, ingawa ni kweli jeni zina uhusiano katika kusababisha kensa ya matiti, lakini mabadiliko kuhusiana na jinsi mtu anavyoishi, pia huweza kuzuaia mtu kupatwa na ugonjwa huo hatari kwa kiasi kikubwa.
Bi. Susan Higginbotham mmoja wa wataalamu hao anasema kuwa, inakadiriwa asilimia 40 ya kesi za ugonjwa wa kensa ya matiti au kesi 70, 000 za ugonjwa huo zinaweza kuzuiwa, nchini Marekani, kwa kufanyika tu mabadiliko ya jinsi watu wanavyoishi.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kula vyakula visivyokuwa na mafuta mengi, kuwa na uzito unaotakiwa kiafya, kuishi maisha yaliyojaa harakati pamoja na kupunguza matumizi ya pombe, bila kusahau kunyonyesha, huweza kusaidia sana katika kutopata ugonjwa wa saratani ya matiti.
Wanasayansi wamehitimisha kwa kusema kuwa, namna mtu anavyoishi ndio suala muhimu sana linaloainisha iwapo mtu anaweza kupata ugonjwa huo au la.
Kwa hivyo, tumeshauriwa kufanya mazoezi kila siku kwa muda usiopungua nusu saa, huku wakinamama wakihusiwa kupunguza kunywa pombe.

No comments: