Saturday, September 5, 2009

Wataalamu wavumbua kingamwili za kuzuia waathirika wa HIV kuelekea katika hali ya Ukimwi


Wataalamu wa Marekani wamefanikiwa kuvumbua kingamwili mbili au antibodies ambazo zinaweza kuzuaia virusi vya HIV visikugawanyika na kuongezeka mwilini, hali itakayopelekea muathiriwa kutoelekea katika hali mbaya zaidi ya ugonjwa huo ya Ukimwi. Uvumbuzi huo ambao ni matokeo ya uchunguzi uliofanyika kwa karibu miongo miwili kuhusiana na virusi vya Ukimwi, unaonekana kuwa ni hatua mihimu inayoweza kupelekea kutengenezwa kinga ya ugonjwa huo. Wataalam hao wamesema kuwa kingamwili hizo zinaweza kutumika kutibu watu walioathirika na ugonjwa wa virusi vya HIV ambao tayari wako katika hali ya Ukimwi.
Uchunguzi huo umefanywa na taasisi ya uchuguzi ya Scripps ya Los Angeles Marekani kwa kutumia sampuli zaidi ya 1,800 za damu za waathiriwa wa Ukiwmi kutoka Thailand, Australia na barani Afrika.

No comments: