Sunday, September 27, 2009

Kusikiliza MP3 kwa sauti kubwa huenda kukakuletea matatizo ya kusikia!


Utafiti unaonyesha kuwa kusikiliza MP3 kwa sauti kubwa kwa saa moja kwa siku, kunaweza kuleta madhara makubwa katika kusikiliza kwa mtu. Kwa mujibu wa utafiti huo, kusikiliza mziki kwa sauti kubwa yawezekana kukapelekea mtu kusikia sauti za ajabu ajabu masikioni.
Uchunguzi uliofanywa na taasisi moja ya wasiosikia umeonyesha kwamba, watu wenye umri wa miaka 16 mpaka 34, husikiliza muziki kwa sauti kubwa bila kujali madhara yake . Wataalamu wanasemakwamba, kusikia sauti kama ya mruzi masikioni, au sauti nyinginezo ni kwa sababu ya kusikiliza mziki kwa sauti kubwa, ambako husababishwa na kuharibika seli za masikio kutokana na sauti kubwa ya mziki na kwa muda mrefu.
Uchunguzi uliofanywa barani Ulaya umeonyesha kwamba, kati ya watu 10 wanaotumia mp3, mmoja kati yao anakabiliwa na matatizo ya kusikia.
Hivo basi wataalamu wanatushauri kutosikiliza mziki kwa sauti kubwa, hasa wakati wa kufanya mazoezi kwa kutumia vifaa vya mazoezi au wakati wa kukimbia, kwani watu wengi kufikiria kuwa kila wanapongeza sauti ya mziki wakati wa mazoezi ndivyo wanavyoweza kuwa na mbio zaidi, suala ambalo si kweli.

No comments: