Saturday, September 26, 2009

Kuna tofauti kati ya lishe ya mwanaume na mwanamke?


Wanaume kwa kuwa na kiasi kikubwa cha misuli, miili yao inahitajia na kutumia vyakula zaidi, au kwa maneno mengine kitendo cha Metabolism katika miili yao chenye maana ya kusaga chakula na kuzalisha nishati, hufanyika zaidi katika miili ya wanaume ikilinganishwa na wanawake. Suala hilo hupelekea wanaume wahitajie nishati (energy), vitamini na madini zaidi kuliko wanawake. Mifupa yao mipana, misuli iliyojengeka, pamoja na mfumo mzimo mzima wa mwili wa mwanaume ni mkubwa zaidi ikilinganishwa na wanawake, na ili kuhifadhi misuli yao wanajitajia kiwango kikubwa zaidi cha protini. Hivyo, wanaume wanahitaji kiasi kikubwa zaidi cha chakula kwa ujumla, ikilinganishwa na wanawake. Wanaume wanahitajia kilokalori 600 zaidi za chakula, kuliko wanavyohitajia wanawake. Hata hivyo kiwango kichotakiwa cha sukari (carbohydrates) na ufumwele (fibires) kwa wanaume ni sawa sawa na kwa wanawake. Hii ni katika hali ambayo wanawake wanahitajia mafuta au fatty acids zaidi kwa asilimia 60 kuliko wanaume.

Uchauri wa kiafya na lishe kwa wanaume:
1. Wanashauriwa kula matunda na mboga mboga kwani vyakula hivyo huilinda miili yao.
2. Wanashauriwa kujiepusha na vyakula vyenye mafuta ya mgando (unsaturated fatty acids) na pia wale nyama nyekundu (red meat) kwa uchache.
3. Wajiepushe kuwa na wasiwasi na mawazo (stress).
4. Wajiepushe na kuvuta sigara na hata kuwwepo katika sehemu zenye moshi wa sigara.
5. Wajitahidi kuwa na uzito unaotakiwa, sio mdogo wala mkubwa sana, kwani uzito mkubwa husababisha mafuta kukusanyika katika mzunguko wa kiuno na tumbo, suala ambalo huongeza hatari ya kupatwa na magonjwa ya moyo.
6. Wasizembee kujishughulisha na michezo na kutunza afya zao.
7. Na mwisho wajiahidi kufanyiwa uchunguzi wa kitiba (check up) kila baada ya muda fulani. Kwani magonja kama kensa ya korodani yanapogunduliwa mapema hutibika kwa urahisi zaidi kuliko yanapocheleweshwa.
…… Haya tena Blog ya Kona ya Afya inawahimiza kinababa wazijali afya zao, kwani kwa kuwa baba ni kichwa cha familia, basi afya na uzima wa kinababa ni muhimu kwa familia na jamii nzima!

No comments: