Tuesday, September 22, 2009

Watoto wenye harakati nyingi hulala kwa urahisi zaidi


Uchunguzi mpya umethibitisha imani ya muda mrefu kuwa pale mtoto anapokuwa na harakati nyingi wakati wa mchana, humsaidia kulala kwa urahisi na mapema zaidi.
Kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa katika makala ya Achieves of Diseases in Childhood, mtoto ambaye hutulia tu na hana harakati yoyote, hupata usingizi kwa taabu na huchukua muda mrefu hadi pale anapolala. Kila saa moja inayotumiwa kwa harakati kama vile kukumbia, inapunguza muda unaotakiwa kwa dakika 6 wa kupata usingizi mtoto. Kila mtoto anapokuwa na harakati ndivyo muda mchache zaidi unavyotakiwa kumafanya alale. Pia imeripotiwa kuwa, watoto wanaopata usingizi kwa haraka, vilevile hulala kwa muda mrefu.
Kulala kwa muda mfupi kwa watoto halikadhalika kumehusishwa na mtoto kuwa mnene sana au obesity. Wataalamu wanasema kuwa, kuwa na harakati mtoto sio tu kwamba ni muhimu sana kwa afya yake, moyo na humfanya awe na uzito unatakiwa bali pia husaidia mtoto aweze kulala vizuri.
Haya akina mama na walezi wote kwa ujumla, msihofu pale mtoto anapokuwa na harakati nyingi na pale wanapocheza sana wakati wa mchana, kwani hilo humsadia kupata usingizi kwa urahisi na kulala vizuri wakati wa usiku. Tusisahau kuwa kipimo cha afya njema ya mtoto ni harakati anazofanya na wala sio kukaa tu kwa utulivu na bila kufanyaa harakati yoyote.
Nakutakieni malezi mema akina baba na akina mama!

No comments: