Monday, March 1, 2010

Kikombe kimoja cha kahawa kwa siku chapunguza hatari ya ugonjwa wa moyo


Mbali na faida kemkem tunazozijua zinazopatikana kwenye kahawa, utafiti mpya umesema kwamba kunywa kikombe kimoja tu cha kahawa kwa siku kunapunguza hatari ya kupatwa na mshituko wa moyo. Utafiti huo uliotolewa katika Kongamano la Jumuiya ya Mshituko wa Moyo la Kimataifa nchini Marekani, umeeleza kwamba kunywa kikombe kimoja cha kahawa ya kawaida na isiyokuwa na kafeini kila siku huzuia kupatwa na mshituko wa moyo kwa asilimia 30. Hata hivyo wataalamu wameonya kuwa kutumia sana kinywaji hicho matokeo yake huweza kuwa kinyume.
Tafiti za huko nyuma pia zilionyesha kuwa, kunywa kila siku kahawa kunaweza kumzuia mtu asipate kisukari aina ya pili na ugonjwa wa akili.
Mpenzi mdau baada ya kufahamu hayo, nimeonea nichukue fursa hii kuelezea baadhi ya faida za kahawa. Mbali ya kawaha kuwa kinywaji murua ambacho kinaweza kukufanya uchangamke asubuhi baada ya kuamka, au kwa wale kina yakhe wanaopenda kuburudika kwa kunywa kahawa kwa kashata vijiweni au kando ya barabara huku wakipiga gumzo, kinywaji hicho kina faida kemkem kiafya
1. Wataalamu wa Chuo Kikuu cha Tiba cha Harvard cha Marekani wamegundua kuwa kunywa kahawa kunazuia kupatwa na ugonjwa wa kibofu nyongo (gall bladder) au kuzuia mawe katika nyongo (gall stones).
2. Kahawa inazuia kupatwa na ugonjwa wa Alzheimer au kusahau hasa uzeeni.
3. Kahawa ina anti-oxidants ambazo hupambana na seli ambaya zinazosabisha saratani.
4. Kahawa hulichangamsha tumbo na kulifanya lifanye kazi vyema na kuzuia matatizo ya kukosa choo. (Bowel stimulant and a laxative).
5. Kahawa huongeza uwezo wa ufahamu wa akili.
6. Kahawa huuzuia ugonjwa wa figo.
7. Na kahawa pia huzuia ugonjwa wa uvimbe wa viungo hasa vikononi na miguuni au gout.
Lakini wataalamu wanatutahadharisha kwamba ingawa kunywa kahawa kuna faida nyingi kama tulivyoona hapo juu lakini haifai kunywa kahawa kwa wingi kila siku. Kwani kila kitu kinachotumiwa sana badala ya kuwa na faida kinaweza kutuletea madhara.
Si vibaya kujua kwamba mmema wa kahawa ambayo ni maarufu uliwenguni kote uligunduliwa mara ya kwanza katika nchi za Yemen, Saudi Arabia na kaskazini mashariki mwa Ethiopia na kwa mara ya kwanza zao hilo lilikuwa likilimwa na kutumiwa sana katika nchi za Kiarabu.

2 comments:

Singa said...

Nashukuru kwa elimu hii. Mimi hupendelea kunywa kahawa kikombe kimoja ninapopatwa na usingizi nikiwa kazini, hivyo hutumia kahawa ili nifanye kazi, nisilale wakati wa kazi. Je kikombe kimoja cha kahawa hakina madhara kwa mama mjazito? Na Je, kuna kitu gani mbadala chaweza kuzuia usingizi, iwapo hutaki kulala wakati wa kazi au wakati unasoma?

Unknown said...

Mwishoa wa ukomo upoje na ipi kawaha sahii