Friday, April 2, 2010

Chokoleti nyeusi zina faida kwa moyo

Japokuwa kumekuwa na mjadala mkubwa kuhusu taarifa kuhusu faida za kiafya za chokoleti, lakini utafiti mpya umedhihirishwa kwamba kula chokoleti nyeusi kuna faida kwa moyo. Utafiti huo uliochapishwa katika jarida la Moyo la Ulaya umeonyesha kwamba, kula kila siku gramu 7.5 za chokoleti, kiasi ambacho ni kidogo kuliko kipande mraba kidogo cha chokolati kunapunguza shinikizo la damu suala ambalo huondoa hatari ya kupatwa na mshituko wa moyo kwa asilimia 39. Kula chokoleti kidogo huweza kumzuia mtu asipate ugonjwa wa moyo lakini iwapo tu italiwa badala ya vyakula vingine viliwavyo katikati ya mlo au asusa (snacks) vyenye kalori nyingi bila kuongeza uzito wa mwili.

Flavanols inayopatikana katika kakao huimarisha uwezo wa kiabiolojia wa seli wa kutengenezwa nitric oxide kuzunguka kuta za damu, suala ambalo hufanya mishipa laini ya damu ipumzike na kupanuka na hivyo kusaidia sana afya ya moyo. Kwa kuwa katika chokoleti nyeusi kuna kakao nyingi, aina hiyo ya chokolati ina taathira kubwa katika kupunguza mfumuko wa mawazo na wasiwasi pamoja (stress) na kusaidia mzunguko wa damu na kiwango cha chinikizo la damu. Lakini inaaminiwa kuwa chokoleti nyeupe hazina kabisa flavanol hivyo hazina faida hiyo.
Wataalamu wamesisitiza kwamba, watu wale chokolate nyeusi kila siku lakini kwa tahadhari kubwa kwani kiasi kidogo tu cha chokolati kina kiasi kikubwa cha kalori na mafuta ambavyo ni hatari kwa afya.

No comments: