Sunday, April 4, 2010

Dawa ya kensa ya tezi kibofu (prostate cancer) yaonyesha matumaini zaidi

Dawa ya kensa ambayo tayari inatumiwa na wagonjwa wenye uvimbe wa tezi za kibofu imeonekana kuwa ina uwezo wa kuzuia ugonjwa huo usiendelee zaidi. Katika uchunguzi wa kimataifa imeonekana kuwa, wanaume waliopewa dawa hiyo ijulikanayo kama Dutasteride katika jaribio la kitiba, wameripotiwa kupungukiwa na hatari ya kupata ugonjwa wa kensa ya tezi kibofu (prostate cancer) kwa asilimia 23. Wanaume wote hao walikuwa wana uwezekano wa kupatwa na ugonjwa huo maishani.

Wataalamu wamepokea kwa furaha matokeo hayo lakini wamesema kwamba bado utafiti wa muda mrefu unatakiwa kufanywa kuhusiana na dawa hiyo.
Huko nyuma pia wataalamu waligundua pia dawa nyingine kama hiyo iitwayo Finasteride inapunguza hatari ya kupatwa na ugonjwa wa kensa ya tezi kibofu lakini baadaye wakaona kuwa inaongeza uwezekano wa kutokea matezi makubwa ya kensa hiyo. Hivyo wamesisiza kwamba inahitajia muda mrefu ili kujua iwapo dawa hiyo haina madhara kabisa.
Inafaa kujua kuwa ugonjwa wa kensa ya tezi kibofu au prostate cancer huwapata wanaume hasa wanapofikia umri wa miaka 50 na wengine katika miaka ya 70. Nchini Marekani pekee mwaka 2005 inakadiriwa kwamba watu 230,000 walipatwa na ugonjwa huo na kusababisha vifo vya watu 30,000. Wanaume wenye matatizo ya shinikizo la damu wanaelekea kupatwa zaidi na kensa ya prostati.

Dalili za ugonjwa wa kenda ya korodani ni:
Kushindwa kukojoa.
Kuona ugumu wakati wa kukojoa.
Kushindwa kuzuia mkojo hasa usiku.
Mkojo kutoka kwa shinda, kuhisi maumivu wakati wa kukojoa.
Kuona damu imechanganyika na mkono na kuhisi maumivu upande wa chini wa kiuno na upande wa juu wa mapaja.
Lakini dalili zote hizo zinaweza kusababishwa na uvimbe wa tezi kibofu ambao hausababishwi na saratani.
Wanaume walio na dalili hizo wanatajwa kumuona daktari na kupata ushauri zaidi.

No comments: