Wednesday, April 21, 2010

Wanamichezo hawapati ugonjwa wa moyo


Utafiti mpya umeonyosha kuwa, kufanya mazoezi kwa muda mrefu hakuhusiana na kuongeza hatari ya kupata ugonjwa wa moyo. Huko nyuma kulikuwa na tafiti zilizoonyesha wasiwasi wa afya ya mishipa ya moyo kwa baadhi ya wanamichezo wa Olimpiki. Tafiti hizo zilisema kwamba, kupanuka kwa mioyo ya wanamichezo kunakoitwa kitaalamu “athlete’s heart” huufanya moyo kuwa dhaifu sana na kushindwa kuvumilia mazoezi mazito.
Lakini kwa mujibu wa uchunguzi uliochapishwa kwenye Jarida la Marekani la Kitengo cha Magonjwa ya Moyo, mazoezi mazito hayana hatari kwa afya ya moyo.
Kiwango cha damu inayosukumwa katika miili ya wanamichezo hakibadiliki wakati wa mazoezi. Mbali na kupanuka kidogo baadhi ya sehemu za moyo, misuli ya moyo hubakia sawa wakati wa mazoezi. Wanasayansi wamehitimisha kwamba, mioyo ya wanamichezo ina afya nzuri na inaweza kuvumilia kirahisi mazoezi ya kiwango cha juu. Pia wamesema kwamba, baadhi ya dawa kama vile erythropoietin (EPO) zinazotumiwa na wanamichezo hao ili kuzipa nguvu chembe chembe nyekundu za damu, kunaufanya utendaji kazi wa moyo udhoofu, suala ambalo limekuwa likiwatokea wanamichezo hao na wala sio mazoezi mazito ya mwili wanayoyafanywa.

No comments: