Thursday, April 1, 2010

Mammography inaweza kuokoa maisha ya wanawake wengi

Japokuwa kumekuwepo na mjadala mkubwa kuhusiana na uwezo wa kutambua ugonjwa wa kipimo kinachotumiwa kugundua kensa ya matiti, lakini utafiti mpya umethibitsiha kwamba, kipimo hicho kina faida kubwa.

Uchunguzi huo umeonyesha kuwa, kipimo cha mammography
faida zake ni kubwa zaidi kuliko hasara zake, na kutumiwa kwakwe kunaokoa zaidi maisha ya wanawake yanayoweza kupotea kutokana na kensa ya matiti. Mammography ina uwezo wa kuonyesha uvimbe (tumors), japokuwa kipimo hicho kinaweza kuonyesha uvimbe ambao hauna madhara, na kuwafanya baadhi ya wanawake kupata wasiwasi na kufanyiwa operesheni bure. Uchunguzi wa huko nyuma ulishauri kuwa, umri wa kufanyiwa kipimo cha mammography ili kujua kama mtu ana saratani ya matiti au la usogezwe kutoka miaka 40 hadi 50 ili kupunguza uwezekano wa wanawake kufanyiwa kipimo hicho mara nyingi maishani, Vilevile imesisitiza kwamba, kwa kila maisha ya mwanamke mmoja yanayonusuriwa kwa kufanywa mammography, kuna wanawake wengine 6 ambao wanafanyiwa kipimo hicho bila ya kuwa na ulazima.
Kwa hivyo wataalamu wamewashauri wanawake wasizembee na kuwahimiza wafanyiwe kipimo hicho, kwani faida yake ni kubwa zaidi kuliko hasara yake.
Nchini Uingereza pekee, zaidi ya wanawake 45,000 hugunduliwa kuwa wana kensa ya matiti kila mwaka, na zaidi ya wanawake 12,000 hufariki dunia kutokana na ugonjwa huo.

No comments: