Wednesday, September 30, 2009

Watoto wa wakinamama wanaofanya kazi hawana afya bora!


Uchunguzi umegundua kuwa watoto ambao mama zao wanafanya kazi, maisha yao ya kiafya ni ya chini ikilinganisha na wale ambao mama zao wako majumbani. Uchunguzi huo uliofanywa na Taasisi ya Afya ya Watoto ya Uingereza umewachunguza zaidi ya watoto 12,500 wenye umri wa miaka mitano na kugundua kuwa watoto ambao mama zao ni wafanya kazi wana harakati kidogo na mara nyingi hula vyakula visivyo salama. Wataalmu hao wamesema kuwa watoto wenye miaka mitano ambao mama zao wanafanya kazi za kudumu au part time, hunywa sana vinywaji venye sukari, katika kipindi cha kati ya milo ya kawaida. Pia hutumia komputa na kuangalia televisheni kwa masaa yasiopungua mawili kwa siku wakilinganishwa na watoto ambao mama zao wako majumbani ambao hutumia chini ya saa moja katika shughuli hizo.
Wataalamu hao lakini wamejitetea kuwa, uchunguzi wao huo haumaanishi kuwa wakinamama wasiende makazini, lakini kunatakiwa kuwepo na sera na mikakati ya kuwasaidi kina mama.

1 comment:

Anonymous said...

ITS TRUE.