Friday, February 26, 2010

Ajifungua watoto wawili baada ya kutolewa ovari na kurejeshewa tena!


Mwanammke mmoja wa Denmark amejifungua watoto wawili salama, baada ya kutolewa ovari za uzazi alipokuwa akiugua kensa, ovari hizo kuhifadhiwa katika barafu na baada ya mwaka mmoja zikarejeshwa tena mwilini mwake. Hadi sasa kuna watoto 8 tu ulimwenguni waliozaliwa baada ya mama zao kurejeshewa ovari, na Stinne Holm Bergholdt ni mwanamke wa kwanza duniani aliyeweza kujifungua mtoto wa pili baada ya ovazi zake kuondolewa na kurejeshwa tena. Bi. Bergholdt aligunduliwa kuwa na ugonjwa wa kensa ya mifupa alipokuwa na miaka 27 na kutokana na hofu ya kutozaa kutokana na athari za tiba ya mionzi na dawa za kensa, aliwataka madaktari wake waondoe ovari zake na kumrejeshea baadaye akipona. Baada ya kupona na mwaka mmoja baadaye alirejeshewa ovari zake na kujifungua mtoto wa kwanza kwa njia ya kupandikizwa mayai katika maabara au Vitro Fertilizertion na kujifungua salama mtoto wa kike aitwaye Aviaja ambaye hivi sasa ana umri wa miaka mitatu. Furaha ya kumzaa mtoto huyo ilimfanya mwamake huyo wa Kidenmark afikirie kuzaa mtoto mwingine. Walipokwenda hospitali ikaonekana kuwa tayari ni mjamzito. Baada ya miezi 9 alijifungua mtoto wa pili wa kike aliyemuita Lucca. Kizazi cha mwanamke huyo kinaendelea vyema na hivi sasa anazuia uzazi ili ajiepushe kushika mimba nyingine.
Taarifa hiyo imeleta matumaini zaidi kwa madakatari na wagonjwa hasa wenye kensa waliokuwa na hofu ya kushindwa kupata watoto hasa baada ya kupata matibabu ya saratani.
Mmh.. suala hili linanifanya nikubaliane zaidi na usemi huu kuwa, Kwa kumtegea Mungu na kwa kupitia sayansi kila kitu kinawezekana!

No comments: