Monday, February 1, 2010

Utoaji mimba usio salama unauwa akina mama elfu sabini kila mwaka


Utoaji mimba usio salama husababisha akima mama elfu sabini kupoteza maisha yao kila mwaka duniani kote. Taasisi mashuhuri ya Guttmacher imeripoti kuwa, japokuwa utumiami wa njia za uzazi wa mpango hupunguza kiwango cha kuharibika kwa mimba, lakini ulimwengu unashuhudia wakinamama wapatao elfu sabini wakifariki dunia kila mwaka kutokana na utoaji mimba usio salama. Imeongeza kuwa, utoaji mimba usio salama unaendelea kuwa tatizo miongoni mwa walimwengu. Imesema kuwa, zaidi ya nusu ya vifo hivyo vya akinamama hutokea katika nchi zilizo chini ya jangwa la Sahara.

No comments: