Saturday, February 13, 2010

Unene unasababisha watoto wa kiume wachelewe kubaleghe


Uchunguzi mpya umeonyesha kuwa watoto wa kiume walio wanene huchelewa kubaleghe kuliko wenzao walio na uzito wa kawaida. Hii ni tofauti na watoto wa kike ambapo unene huwasababishia hufikia baleghe mapema. Huko nyuma pia wataalamu walisema kwamba, kuna uhusiano kati ya BMI na kubaleghe mapema watoto wa kike na kuongeza kwamba, suala hilo kusababishwa na kuongezeka kwa homoni inayojulikana kama Leptin kwa watu wanene. Uchunguzi mpya umesema homoni hiyo hiyo husababisha watoto wa kiume walio wanene wachelewe kubaleghe. Kuna uwezekano kuwa homoni hiyo inageuza homoni za kiume na kuwa za kike katika tishu za mafuta na kusababisha watoto wa kiume wachelewe kukubaleghe.
Kwa upande mwingine utafiti mpya umesema kwamba, unene huanza kabla ya mtoto kufikia miaka miwili. Utafiti huo uliofanywa na wataalamu wa Marekani umesema kwamba, unene ambao huweza mtu kuwa nao katika umri wake wote huanza wakati anapokuwa na miaka miwili. Uchunguzi huo uliowafanywa kwa kuwahusisha watoto wanene 100 na vijana umegundua kwamba, nusu ya watoto hao walikuwa wanene walipokuwa na miezi 24 na kwa asilimia 90 walikuwa ni wenye uzito mkubwa walipokuwa na miaka mitano.
Si vibaya kujua kuwa nchini Uingereza asilimia 27 ya watoto wa nchi hiyo ni wanene. Ingawa sababu hasa inayopelekea watoto wawe wanene mapema katika umri wao haijajulikana lakini wataalamu wanasema kwamba lishe mbovu, kuanza kupewa watoto vyakula vigumu mapema pamoja na kutofanya mazoezi mapema na kujibweteka ni mausala yanayochangia watoto kuwa wawe na unene wa kupindukia tangua wakiwa wadogo.

No comments: