Wednesday, February 17, 2010

Dawa za Herpes zinaweza kuwasaidia wagonjwa wa UKIMWI


Utafiti mpya umeonyesha kwamba, dawa zinazotumiwa kutibu ugonjwa wa Herpes au ugonjwa wa malengelenge neva ngozini kwa Kiswahili, zinaweza kuwasaidia pia waathirika wa HIV ili wasianze kutumia dawa ya ARV mapema. Kwa mujibu wa utafiti huo uliochapishwa katika jarida la Lanset, dawa hizo zinazoitwa Acyclovir husaidia kupunguza uwezekano wa Ukimwi kushika kasi kwa asilimia 16 kwa mgonjwa. Hata hivyo kutumiwa Acyclovir hakupunguzi maambukizo ya HIV kwa watu wengine, na wataalamu wamesisitiza kwamba dawa za kurefusha maisha ya waathiriwa wa Ukimwi au antiretroviral drugs zina athari zaidi kuliko dawa hiyo ya acyclovir katika kuudhibiti Ukimwi. Madakatari wanasema kwamba, dawa hiyo ambayo haigharimu fedha nyingi inafaa kuokoa maisha ya waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi, na kuongeza muda kabla ya kuanza kutumia dawa nyinginezo ambazo ni ghali.
…Tukishirikiana pamoja tutaushinda Ukimwi!

No comments: