Wednesday, April 7, 2010

Cheka unenepe na uishi maisha marefu


Utafiti mpya umeonyesha kwamba, kuna uhusiano kati ya kucheka na kuishi maisha marefu.
Utafiti huo uliochapishwa katika Jarida la Saikolojia la Sayansi umeonyesha kwamba, watu wenye tabasamu pana linalojulikana kama "Dunchenne smile, huishi maisha marefu. Ernest L. Abel aliyeongoza utafiti huo amesema kwamba, watu ambao wanaonyesha hisia zao na kuziakisi kwa tabasamu pana, kimsingi huwa ni watu wenye furaha zaidi ya wale wenye kutabasamu kidogo. Hivyo watu hao hufaidika na suala hilo na kwa kawaida huishi maisha marefu.
Wataalamu wanasema kwamba watu wenye kutabasamu sana kwa kawaida huwa wana furaha, wana shaksia madhubuti, ndoa zao hudumu zaidi, wana ufahamu mzuri zaidi wa mambo na huashiriana vyema na watu wengine.

1 comment:

Unknown said...

hahahahahahhah kwikwikwikwi yani ni kucheka tu hapa