Saturday, February 14, 2009

Kufanya mazoezi huzuia kupata kensa ya tumbo


Inaaminika kuwa kufanya mazoezi kunaweza kupunguza uwezekano wa kupata kensa ya tumbo (Bowel cancer). Wataalamu wa Marekani baada ya kufanya uchunguzi wamegundua kuwa, mazoezi ya aina mbalimbali kama vile kukimbia na kwenda gym kunaweza kupunguza uwezekano wa kupata kensa ya tumbo kwa asilimia 25.
Wanasema kuwa, kuwa na kiasi cha kawaida cha uzito ni moja ya njia za kupunguza uwezekano wa kupata kensa ya matumbo na kensa nyinginezo, suala ambalo linaweza kupunguza uwezekano wa kutokea kesi karibu 13,000 za ugonjwa huo duniani kila mwaka.
Tukumbuke kuwa, kensa inayoathiri utumbo mkubwa ni moja ya kensa hutokea zaidi katika kensa za tumbo.
Haya shime kufanya mazoezi ili tuzilinde afya zetu!

No comments: