Thursday, February 12, 2009

Nadharia ya kuzaa watoto nane kwa mpigo (Octuplets


Mwanamke mmoja wa kimarekani amejifungua watoto nane huko California, ikiwa ni baada ya muongo mmoja tangu mwanamke mmoja wa Nigeria kujifungua kwa mara ya kwanza watoto nane hai duniani. Wataalamu wanasema suala la kuzaa watoto nane kwa mpigo linatokea kwa nadra sana na ni matukio kadhaa tu kama hayo yaliyoweza kutokea dunia, ambapo mpaka sasa hakuna watoto mapacha nane waliowahi kuishi baada ya kuzaliwa. Lakini watoto mapacha nane waliozaliwa huko California na mwanamke aitwaye Nadya Suleman wako hai na wanaendelea kuishi bila matatizo yoyote muhimu ya kiafya.
Lakini suala kubwa la kujiuliza hapa ni kuwa, suala hilo huweza kutokea vipi?
Mimba za mapacha za aina hiyo hutokea kwa nadra sana kwa njia ya utungwaji wa mimba wa kawaida. Mimba za mapacha wengi mara nyingi hutokea iwapo zimetumiwa dawa za kuyapa nguvu mayai ya mwanamke kwa lengo la kuzaliwa mayai mengi ili mwaname aweze kushika mimba kwa urahisi. Wanawake wanaobeba mimba kwa njia hiyo, huangaliwa kwa karibu na madaktari wao ili kuhakikisha kuwa mayai mengi hayazaliwi na kukua, na kama yakizaliwa basi hushauriwa kutobeba mamba kwa kujizuia kujamiana au kutumia njia za kuzuia mamba. Suala hilo huzuiliwa kwani mimba pacha za watoto wengi huhatarisha maisha ya mama na vichanga. Hii inamaanisha, kila kiwango kidogo cha watoto kinapokua katika mfuko wa uzazi wa mwanamke mjamzito ndio fursa nzuri inavyopatikana ya kukua vizuri watoto tumboni mwa mama. Kwa upande mwingine mama mjamzito kila anavyozidi kuwa na watoto wengi tumboni ndio matatizo kama vile kupata shinikizo la damu, kifafa cha mimba na sukari wakati wa ujauzito ndivyo yanavyoongezeka.
Hata hivyo watoto mapacha nane wa California wamezaliwa vizuri tu, ingawa wamezaliwa kabla ya umri wao kutimia, yaani wakiwa (premature) lakini wamezaliwa na uzito ambao si mdogo sana. Tusisahau kuwa mama huyo alikuwa akiangaliwa vyema na madaktari kabla ya kujifungua, na alijifungua kwa operesheni iliyofanywa na timu ya makumi ya madaktari wakihakikisha kuwa, vichanga hivyo vinazaliwa salama salimin.
Link….http://news.bbc.co.uk/2/hi/health/7853257.stm

No comments: