Wednesday, February 25, 2009

Onyo kwa wanawake wanywaji!



Wanawake wanaopendelea kunywa mvinyo kila usiku wameonywa kwamba, wako katika hatari kubwa ya kukabiliwa na kensa!
Watafiti wa Kensa wa Uingereza wametangaza kwamba, kunywa gilasi moja tu ya ulevi kwa siku kunasababisha kensa 7,000 za ziada, nyingi zikiwa ni za matiti, hasa kwa wanawake wa nchi hiyo.
Hatari ya kupata ugonjwa huo inaongezeka kila unywaji unavyoongezeka, na hakuna tofauti iwapo pombe hiyo ni spirits, mvinyo au bia ya Safar Lager!. Hayo ni kwa mujibu wa watafiti hao. Takwimu zimeonyesha kuwa, kunywa pombe chupa moja kwa siku kunaongeza uwezekano wa kupata aina zote za kensa kwa asilimia 6 kwa wanawake ambao wana umri wa mpaka miaka 75.
Haya chime kina mama wanyaji, msijisahau na mjali afya zenu!
Link..
http://news.bbc.co.uk/2/hi/health/7906355.stm

No comments: