Saturday, February 21, 2009

Kuvuta sigara katika umri mdogo kunasababisha ugonjwa wa MS


Watu ambao wanaanza kuvuta sigara wakiwa katika umri wa kabla ya miaka 17, wako katika hatari ya kupatwa na ugonjwa wa Multiple Sclerosis au MS. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa katika mkutano wa 61 wa kila mwaka wa Taasisi ya magonjwa ya mishipa ya fahamu ya Marekani, zaidi ya asilimia 32 ya wagonjwa wa MS walikuwa ni wale walioanza kuvuta sigara katika umri mdogo. Utafiti huo umeonyesha kuwa, wanaovuta sigara katika umri mdogo wana uwezekano wa kupata ugonjwa wa MS mara 2.7 zaidi ya wengine. Utafiti huo lakini haukuonyesha kuwepo hatari hiyo kwa wale wanaoanza kuvuta sigara wakiwa na umri mkubwa. Ugonjwa wa multiple sclerosisi ni ugonjwa wa mfumo wa kinga ya mwili ambao hutokea pale mfumo huo unaposhambulia mfumo wa kati wa fahamu ( central nervous susytem), hali ambayo hupelekea seli za fahamu kushindwa kuwasiliana. Ugonjwa huo mara nyingi huanza kwa kupoteza hisia mbalimbali mwilini kama kuona, kuhisi, kushindwa kutembea, kupumua na mwishowe kupooza mwili mzima.
Shime tuungane kupinga vijana kuanza kuanza kuvuta sigara katika umri mdogo!

No comments: