Wednesday, February 11, 2009

Kula mayai kwa kiasi unachotaka hakuna madhara?


Uchunguzi umethibitisha kwamba kula mayai kwa kiasi cha kawaida kuna athari ndogo katika kuongeza kiasi cha kolestiroli mwilini. Timu ya wataalamu wa Surrey waliofanya uchunguzi huo wanasema kwamba uchunguzi wao umeonyesha kuwa watu wanaweza kula mayai kwa kiasi wanachotaka bila kuathiri afya zao. Wataalamu hao ambao wameangalia chunguzi kibao kuhusiana na lishe inayotokana na mayai wamesema kuwa, suala kuwa kula zaidi ya mayai matatu kwa wiki kunaleta madhara, limezoeleka lakini suala hilo si sahihi na ni kwa mujibu wa taarifa zilizopitwa na wakati. Ukweli ni kuwa kiasi cha kolestiroli (mafuta) kinachopatikana katika mayai kwa kawaida hakichangii kwa kiasi kikubwa katika kiasi cha kolestiroli ya damu yako.
Haya jamani shime kula mayai katika milo yetu ya kawaida na shime tupinge dhana potofu kuwa mama mjamzito haruhusiwi kula mayai, kwani mama mjamzito anatakiwa kula vyakula vyote katika lishe bora na ilojitosheleza.
Link…. http://news.bbc.co.uk/2/hi/health/7882850.stm

No comments: