Monday, February 16, 2009

Matibabu ya Ukimwi kwa kutumia jeni yaleta matumaini


Matokeo ya jaribio la kutumia jeni (gene) kutibu ugonjwa wa Ukimwi limeleta matumani kuhusiana na tiba ya ugonjwa huo hatari. Baada ya jaribio hilo kufanywa kwa wagonjwa 74, imeonekana kuwa tiba hiyo ni salama na inaweza kupunguza madhara ya virusi vya HIV katika mfumo wa ulinzi wa mwanadamu yani Immune system. Wataalamu wanasema kuwa, kwa kutumiwa njia hiyo tiba moja tu ya jeni itakuwa inatosha badala ya mgonjwa wa ukimwi kutumia vidonge vinavyopunguza makali ya ugonjwa wa Ukimwi ambavyo inambidi muathiriwa avitumie umri wake wote. Jaribio hilo la kitiba pia limeonyesha kuwa, wagonjwa waliotumia tiba hiyo ya jeni miili yao ilikuwa na seli za CD nyingi zaidi. Hata hivyo tiba hiyo bado inachunguzwa ili kuhakikisha kuwa ni salama kutumiwa.
Tumuombe mola awezeshe tiba hiyo iwe salama na itumike ili kuwapunguzia maumivuu na mahangaiko wagonjwa wa ukimwi!
Link…. http://news.bbc.co.uk/2/hi/health/7883023.stm

No comments: