Monday, February 23, 2009

Kunywa maji, ni muhimu kwa mwili wako!


Je unajua asilimia 75 ya mwili wako ni maji? Na kama unajua, je unajua pia robo tatu ya uso wa dunia ni maji? Sawa pengine ukawa hilo unajua, lakini je, unajua pia maji ni kimiminiko muhimu katika kusafirisha chembechembe muhimu mwilini mwako? Vilevile ujajua kuwa kuna lita 42 za maji mwilini mwako na iwapo utapoteza lita 2.7 tu ya maji hayo basi uko hatarini kupungukiwa na maji mwilini?
Halikadhalika je, unajua kuwa, ukosefu au upungufu wa maji mwilini huweza kukusababishia matatizo kibao, kama vile kuchoka, kuwa na wasiwasi na hasira, kusikia kizunguzungu, udhaifu, maumivu ya kichwana mengineyo mengi?
Hii inaonyesha umuhimu wa maji mwilini mwako na kwa viumbe hao wote wanaotuzunguka.
Basi kunywa maji, ila usisahau kunywa maji safi na salama!

No comments: