Friday, February 27, 2009

Wanaume wanashauriwa kumeza vidonge vya kuzuia kensa ya korodani( prostate cancer)


Kwa mara ya kwanza madaktari wameshauri wanaume kutumia baadhi ya dawa kwa lengo la kujikinga na ugonjwa wa kensa ya korodani.
Lakini wanume hao ni wale tu ambao wako katika hatari ya kukabiliwa na ugonjwa huo. Yaani wako at risk. Hawa ni wale ambao ndugu zao wa karibu kama baba, babu au hata kaka na baba mdogo wamepatwa na ugonjwa huo wa kensa ya korodani.
Ugonjwa wa kensa ya korodani ni ugonjwa unaosababisha buje au tumor inayokua polepole katika korodani zao (tests), buje ambalo huweza kujulikana tu kwa kufanya kipimo cha biopsy baada ya mgonjwa kupimwa na damu yake kutiliwa wasiwasi katika kipimo cha PSA.
Maelekezo mapya yaliyotolewa na Jumuiya ya magonjwa ya Saratani na Matatizo yanayoambatana na mfumo wa mkojo ya Marekani ni kuwa, kila mwanamme aliye hatarini ni bora atumie dawa aina ya FINESTERIDE (PROSCAR) bila kujali kuwa dawa hiyo inaweza kuwa na madhara kidogo(side effects).
kwani dawa hiyo inazuia kupatwa na kensa ya korodani kwa asilimia 25.
Dawa ya Finesteride hivi sasa inatumika kutibu baadhi ya magonjwa mbaliambali yanayoambatana na matatizo ya mkojo.
Wanasayansi wanaamini kuwa, dawa hiyo inamkinga mtu na maradhi ya kensa ya korodani kwa kupunguza ukubwa wa korodani na kupunguza kiwango cha homoni ya testosterone.
Haya shime kwa wanaume wote wanaokabiliwa na ugonjwa wa kensa ya korodan, kumbuka kuwa kukinga siku zote ni bora kuliko kutibu.
Tutazungumzia kensa ya korodani katika siku za mbele. Kama kawaida nawahusia kuzijali afya zenu!

No comments: