Sunday, October 25, 2009

Marekani yatangaza homa ya mafua ya nguruwe kuwa janga la kitaifa


Rais Barack Obama wa Marekani ametangaza kuwa homa ya mafua ya Nguruwe ni janga la kitaifa. Taarifa kutoka ikulu ya White House imesema kuwa Rais Obama alitia saini hati ya tangazo hilo usiku wa Ijumaa. Tangazo hilo litapelekea kuongezwa mikakati ya kupambana na homa hiyo aliogunduliwa mapema mwezi Aprili mwaka huu nchini Mexico. Duru za habari zinaarifu kuwa takriban majimbo 46 ya Marekani yameathiriwa na homa hiyo huku zaidi ya Wamarekani 1000 wakiripotiwa kuaga dunia kutokana na virusi vya H1N1 vinavyosababisha homa ya mafua ya nguruwe. Rais Obama amesema kuwa ugonjwa huo unasambaa kwa kazi na hivyo pana haja ya kuongeza juhudi za kukabiliana nao. Kutiwa saini hati ya tangazo hilo kunaipa serikali idhini ya kuepuka masuala ya kiitifaki katika kukabiliana na ugonjwa huo.

No comments: