Friday, October 16, 2009

Wanawake 70 elfu hufariki dunia kila mwaka kutokana na utoaji mimba usio salama


Ingawa njia za kuzuia mimba hupunguza utoaji mimba holela kwa kiasi kikubwa, lakini ulimwengu unashuhudia wanawake 70 elfu wakipoteza maisha yao kila mwaka kutokana na kutumia njia zisizo salama kutoa mimba. Ripoti zinasema kuwa hata hivyo kiwango cha utoaji mimba kimepungua duniani ikilinganishwa na miaka ya nyuma. Katika nchi ambazo kumekuwa na sheria kali za kuzuia utoaji mimba, kumeshuhudiwa utoaji mimba wa kutumia njia siziso salama kwa afya ya mama ukiongezeka zaidi.
Hata hivyo bado takwimu zinaonyesha kuwa, utoaji mimba holela umeendelea kuwa tatizo sugu linalogharimu maisha ya wanawake 70,000 kila mwaka duniani. La kusikitisha zaidi ni kuwa vifo hivyo hutokea zaidi katika nchi zilizoko Afrika chini ya jangwa la Sahara.
Wakinamama na wanawake wanapaswa kujua kuwa, utoaji mimba holela na kwa kutumia njia zisizo salama zaidi ya kuhataraisha maisha ya mwanamke, humsababishia pia matatizo mbalimbali ya kiafya na pengine hata kupelekea asiweze tena kubeba mimba baadaye.
Ni muhimu kwa baba na mama kupanga uzazi ili kuboresha maisha ya familia zao na pia kulinda maisha ya mama. Chambelecho waswahili : kukinga siku zote ni bora zaidi kuliko kuponya"!

No comments: