Saturday, October 31, 2009

Obama aondoa marufuku ya kuingia nchini Marekani walioathiriwa HIV


Marekani imeondoa marufuku ya kuingia nchini humo watu walioathiriwa HIV, sheria ambayo imetumiwa kwa miaka 22. Rais Barack Obama amethibitisha kuondoalewa marufuku hiyo wakati akiongeza fedha kwa ajili ya kuimarisha huduma za magonjwa yanayoambatana na ugonjwa wa Ukimwi na HIV. Akibatilisha sheria hiyo Obama amesema kuwa, iwapo nchi hiyo inataka kuwa kiongozi katika kukabilina na Ukimwi basi wanapaswa kufanya vitendo kama hivyo. Ameongeza kuwa kuwapiga marufuku kuingia Marekani watu wenye Ukimwi kumetokana na woga badala ya kukubali ukweli wa suala hilo.
Marekani ilikuwa miongoni mwa nchi chache duniani ambazo zinazuia watu wenye Ukimwi kuingia katika nchi hizo. Sheria hiyo mpya inatarajiwa kuanz akutumika mwanzoni mw amwaka 2010.

No comments: