Monday, October 26, 2009

Wanawake wana dalili sawa za mshituko wa moyo na wanaume


Imekuwa ikiaminiwa kuwa wanawake wanapatwa na mshituko wa moyo tofauti na wanaume lakini wataalamu wamegundua kuwa fikra hiyo haina ukweli wowote. Wataalamu wa Magonjwa ya Moyo wa Canada wamesema hayo baada ya baada ya kuchunguza wanawake 305 waliokuwa wakifanyiwa operesheni ya angioplasty. Wataalamu hao wamesema kuwa, ugonjwa wa moyo huwapata kwa dalili sawa wanawake na wanaume. Mwaka 2003 Taasisi ya Kitaifa ya Marekani ilitangaza kwamba, wanawake wengi hawapatwi na maumivu ya kifua wakati wanapopatwa na mshituko wa moyo, na dalili za ugonjwa huo kwa wanawake hutofautiana. Lakini wataalamu wa Canada wamegundua kuwa, wanawake pia kama wanaume huhisi dalili za kawaida za mshituko wa moyo kama vile maumivu ya kifua pamoja na mauamivu katika koo, taya na shingo. Wamesema kuwa, taarifa zilizo sahihi zinapaswa kufikishiwa jamii ili kuhakikisha kwamba wanawake pamoja na wataalamu wa vituo vya afya wanatambua kuwa dalili muhimu za mshituko wa moyo ziko sawa kwa wanawake na wanaume.
Inafaa kujua kuwa dalili za tahadhari za kupatwa na mashituko wa moyo ni:
 Kuhisi maumivu kifuani
 Kushindwa kupumua
 Kuhisi kichefuchefu
 Kutokwa jasho
 Kuhisi wasiwasi

No comments: