Wednesday, October 7, 2009

Nani kasema Maharagwe si Mboga?


Mie naamini maharagwe ni mboga tena yanaweza kuwa ni mboga zaidi
kuliko hata mboga nyinginezo zinazoliwa kama mboga. Hii inatokana na ukweli unaotokana na faida tele na muhimu zinazotokana na chakula hicho. Wataalamu wanatuambia kuwa katika kila gramu 100 za maharagwe tunaweza kupata gramu 22 za protini, gramu 6 za madini ya chuma, miligramu 1370 za Potassium na mikrogramu 130 za Folic Acid.
Si vibaya pia ukijua kwamba, kuzoea kula maharagwe kila mara kunazuia hatari ya kupatwa na magonjwa ya moyo kwani husaidia kupunguza kiwango cha mafuta aina ya Colestrole mwilini. Kwani maharagwe yamejaa protini na ufumwele (Fibres) ambazo husaidi sana katika suala hilo.
Halikadhalika kwa wale wanaotaka kupunguza uzito maharagwe ni miongoni mwa vyakula wanavyoshauriwa kula.
Pia ni miongoni mwa vyakula vinavyosaidia katika kupunguza uwezekano wa kupata kisukari.Bila kusahau kuwa maharagwe huongeza kiwango cha mada iitwayo Leptin mwilini, ambayo hukufanya usitamani kula (appetite reducer), kinyume na vyakula vyenye sukari ambavyo kila unapokula leptin huzalishwa kwa kiwango kidogo mwilini na kukufanya utake kula zaidi.
… ndio sababu basi nikasisitiza tena na tena kuwa….Maharagwe ni mboga, tena mboga iliyo bora!

2 comments:

Mzee wa Taratbu said...

Hamna mboga nzuri kwangu na tamu kama maharagwe yani.

Shally's Med Corner said...

Nakubaliana na wewe Mzee wa taratibu!