Wednesday, January 27, 2010

Bill Gates aahidi ulimwengu kupata kinga ya Malaria miaka mitatu ijayo


Bill Gates mgunduzi wa Microsoft amesema kwamba kinga ya Malaria itakuwa tayari baada ya miaka mitatu ijayo. Gates anaongoza kampeni za kupambana na ugonjwa wa Malaria, ambao unasababisha vifo vya mamilioni ya watu duniani kila mwaka hasa watoto wadogo. Bili Gates anaamini kuwa kama ilivyokuwa kwa ugonjwa wa ndui, Malaria pia inaweza kutokomezwa. Hata hivyo mpaka hivi sasa hakujapatikana kinga yoyote ya ugonjwa huo, lakini Gates ana matumain kwamba kinga hiyo itagunduliwa hivi karibuni. Gates ambaye ameunda taasisi inayotumia mabilioni ya dola kupambana na ugonjwa wa Malaria, amesema kuwa hivi sasa kuna kinga ambayo inafanyiwa majaribio ya mwisho, na kinga ya muda inaweza kuanza kupatikana baadaya miaka mitatu, lakini kinga kamili ya ugonjwa huo itaweza kuchukua hadi miaka 10 kutengenezwa. Hata hivyo Gates ambaye anaaminika kuwa tajiri zaidi duniani, ametahadharisha kwamba, ana wasiwasi nchi zinazoendelea zitatumia fedha zao zote zinazotokana na misaada ya kigeni katika kukabiliana na madhara ya mabadiliko ya hali ya hewa, na kupuuza masuala ya afya. Gates amesema kwa mtazamo wake suala hilo ni makosa na kwamba viongozi wa nchi zinazoendelea wanapaswa pia kuboresha hali ya afya ya wananchi wao na kwa upande mwingine kujitahidi kudhibiti kukua kwa idadi ya watu, suala ambalo lina athari kubwa kwa mabadiliko ya hali ya hewa.
 Malaria ni moja ya magonjwa yanayosabaisha vifo vingi sana duniani hasa katika bara la Afrika.
 Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani, ugonjwa huo unasababishwa vifo vya watu kati ya milioni 1.5 hadi 2.7 kila mwaka duniani. Watoto walio chini ya miaka mitano ndio wanaoathirika sana na ugonjwa huo, huku zaidi ya watu milioni moja wakifariki kila mwaka barani Afrika kutokana na ugonjwa wa Malaria.
 Miongoni mwa vimelea vinavyosababishwa ugonjwa wa Malaria Plasmodium Falciparum ndio kijidudu inachosababisha malaria mbaya zaidi, na kila uchao kimeleo hicho huzidi kukwepa dawa za malaria na kujiimarisha.
 Si vibaya kutambua kwamba, Malaria inauwa watu 8,000 nchini Brazil kila mwaka, hii inamanaisha kwamba ugonjwa huo unaua watu wengi zaidi nchini humo ikilinganishwa na idadi ya watu wa nchi hiyo wanaokufa kutokana na UKIMWI pamoja kipindupindu.
 Gharama inayotumika kutibu ugonjwa wa Malaria barani Afrika kwa mwaka ni zaidi ya dola bilioni 3.

2 comments:

JONAS TINGATINGA said...

I will be there waiting for it. Naichukia Maralia now and then. Die yourself you stupid Malaria Leave us alone with joyfully world.

Tingatinga jonas

JONAS TINGATINGA said...

I will be there waiting for it. Naichukia Maralia now and then. Die yourself you stupid Malaria Leave us alone with joyfully world.

Tingatinga jonas