Wednesday, January 13, 2010

Kuangalia televisheni muda mrefu kunapunguza umri


Utafiti wa hivi karibuni umeonyesha kwamba kuangalia televisheni kwa zaidi ya masaa mnne kwa siku kunapunguza umri. Wataalamu wa Australia wamegundua kwamba, watu ambao hukaa kwa muda mrefu wakitazama televisheni, wanakabliwa na hatari kubwa ya kupatwa na matatizo ya afya hasa magonjwa ya mishipa ya damu, suala ambalo huhatarisha maisha yao na kuwapunguzia umri. Wanasema kwamba, kukaa muda mrefu mbele ya TV kuna hatari kubwa kwa maisha ya mtu kutokana na kuwa shughuli za kawaida za mtu ambazo ni pamoja na kusimama na kutumia misuli ya mwili huwa hazifanywi na mtu hukaa tu chini. Wataalamu hao wameelezea kuwa, watu wengi kwa siku hujongea tu kutoka kiti kimoja hadi kingine, kutoka katika gari kuelekea ofisini na kutoka katika kiti cha ofisini hadi nyumbani katika kiti kingine mbele ya televisheni.
Uchunguzi huo umetahadharisha kwamba, hata watu wenye afya zao za kawaida wanaweza wakawa wanakabiliwa na hatari kubwa kutokana na kukaa kwa muda mrefu suala ambalo huathiri kiwango cha sukari na mafuta katika damu. Hatari ya kukaa kwa muda mrefu haiwezi kuondolewa kwa kuanza kufanya mazoezi, kwani uchunguzi huo umegundua kuwa, hata watu wanaofanya mazoezi, iwapo wanaangalia tv kwa muda mrefu, pia wana hatari ya kuwa na maisha mafupi.

1 comment:

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Wallahi ukifuata kila kitu wanachosema hawa wanayansi utashindwa kuishi! Kazi kwelikweli.